Skip to main content

TAARIFA KAMILI KISII

-Ni wakati wa kupokea habari za yard fm na AGR FM, abagusii global radio lakini kwanza tupate mkhutasari wake.

Naomba makanisa mjitolee tuombee nchi yetu -asema dakari Nyandoro
-Mbunge wa Nyaribari Masaba Elijah Moindi  asema shule zizawadiwe baada ya kufanya vyema katika  mitihani
-Wakaazi wa kisii waombwa kumpa gavana ongwae mda kufanya maendeleo.
-Wanaochimba barabara wakamatwe na kushtakiwa asema mbunge Timothy Bosire
HABARI KAMILI:

1 Makanisa yote yameombwa kuombea nchi ya Kenya ili kuwe na amani na kuzuia visa vya mashambulizi kuendelea kushuhudiwa nchini.
Akiongea jana katika hafla ya kuchangisha fedha za ujenzi wa kanisa ya kiadventista ya Tindereti iliyoko eneo bunge la Borabu kaunti ya Nyamira daktari Yobesh Kambi aliomba wahumini wa makanisa mbalimbali kuendelea kuombea nchi ya Kenya ili amani iendelee kushuhudiwa.
Wakati uo huo, daktari Nyandoro aliomba wakaazi kushirikiana pamoja kuleta maendeleo katika jamii ya mkisii haswa katika kaunti ya Nyamira.
Hii  ni baada ya kaunti ya Nyamira kusemekana kuwa imerudi nyuma kimaendeleo  jambo ambalo viongonzi wengi kutoka kaunti hiyo hawajafurahishwa nalo huku viongonzi wengi wakshtumu uongonzi ulioko katika kaunti hiyo .
2 Mwanafunzi mmoja wa umri wa miaka 17 katika shule ya upili ya Mariindi iliyoko  kaunti ya Nyamira kwa jina Judy Maasi amejitoa uhai wake baada ya kujirusha ndani ya choo ya shule hiyo yenye futi 60 leo asubuhi.
Akitibithisha kisa hicho OCPD wa kaunti ya Nyamira Ricah Ongare alisema mwanafunzi huyo aliyekuwa kidato cha tatu katika shule hiyo ya Mariindi alijirusha ndani ya choo leo mwendo wa saa 6:00 asubuhi baada ya kupatikna  akiwa katika bweni ya shule hiyo akiongea na simu usiku wa kuamkia leo jambo ambalo ni kinyume na sheria za shule hiyo.
Inasemekana msichana huyo aliamua kujitoa  uhai kwa kuogopa kuwa angechukuliwa hatua kwani alipatikana akiongea na simu usiku wa kuamkia leo na mwalim mmoja wa shule hiyo anayesimamia wanafunzi ambao wanaishi katika mabweni ya shule hiyo.
Mwili wa marehemu huyo umetolewa kwa choo hiyo na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Nyamira.
3 Mbunge wa eneo bunge la Nyaribari Masaba kaunti ya Kisii Elijah Moindi amesema shule ambazo zitafanya vyema katika mitihani ya kitaifa kutoka eneo bunge lake atazizawadi kama njia mojawapo ya kuwatia motisha walimu pamoja na wanafunzi.
Akizungumza jana katika  eneo bunge lake  mbunge huyo alisema  shule zote ambazo zitafanya vizuri katika mitihani ya kitaifa atahakikisha zimezawadiwa kati ya walimu pamoja na wanafunzi kama njia mojawapo ya kuinua viwango vya elimu juu zaidi katika eneo bunge lake.
Aidha mbunge huyo alisema baada ya shule ya upili ya wasichana ya St Charles Ichuni Lwanga amboyo iko katika bunge lake na ambayo iliweza kufanya vizuri  katika mtihani wa kidato cha nne mwaka jana siku ya jumatatu ataikabidhi shule hiyo gari [school bus] ili iwe funzo kwa shule zingine kutia motisha.
Shule hiyo ya wasichana kutoka bunge lake ilifanya vizuri na kuorodheshwa miongoni mwa shule ambazo ziliweza kufanya vizuri katika kaunti ya kisii.
4 Mbunge wa Kitutu Chache kaskazini kaunti ya Kisii Jimmy Angwenyi amewaomba wakaazi wa kaunti ya Kisii kumpa gavana wa kaunti hiyo James Ongwae mda zaidi ili kutimiza miradi aliyo nayo kwa kaunti yake.
Akizungumza katika uga wa shule ya upili ya wasichana ya Marani iliyoko eneo bunge lake wakati wa hafla ya mazishi ya mfanyikazi wa mbunge huyo, mbunge huyo alisema kuna haja ya wakaazi kumpa gavana wakati mwafaka kutimiza miradi aliyo nayo katika kaunti ya Kisii
Wakati huo huo, viongonzi waliohudhuria hafla hiyo kutoka kaunti ya Kisii walihapa kufanya kazi pamoja ili viwango vya maendeleo kuinuka zaidi.
Viongonzi waliohudhuria hafla hiyo ni gavana Ongwae, mbunge wa Kitutu Chache Kusini Richard Onyonka, Seneta mteule kaunti ya Kisii Hosea Onchwang’i, wawakilishi wa wadi mbalimbali za kaunti ya Kisii pamoja na wananchi wote kwa jumla.
5 Mbunge wa eneo Bunge la Kitutu Masaba, Kaunti ya Nyamira Timothy Bosire amewaomba Askari wa utawala na Machifu kufanya uchungunzi kuhusu wale wana tabia ya kulima na kupanda mgomba wa ndizi kwenye barabarza eneo bunge hilo.
Akiongea  katika shule ya upili ya Rigomba iliyoko eneo bunge lake iliyochomeka mwenzi moja uliopita na kuifadhili Sh900,000 ili kujenga bweni mpya, Mbunge Bosire aliwaomba Askari pamoja na machifu kuwakamata na kuchukuliwa hatua za Kisheria wanaochimba barabara wakidai ni njia moja ya kulalamikia barabara mbovu.
Wakati uo huo,  Mbunge huyo aliwakosoa vikali wale wanafanya uharibifu huo wa barabara na kusema ni kukiuka sheria za nchi ya Kenya
6 Wakaazi wa kaunti ya Kisii wamehimizwa kupanda miti kama njia moja ya kutunza mazingira huku wakishauriwa kuhakikisha kuna usafi kila mahali ili kuepukana na mkurupuko wa magonjwa kama vile kipindupindu.
Akiongea katika shule ya msingi ya Kisii wakati wa kuadhimisha siku ya mzingira ulimwenguni, msimamizi wa mkahawa wa Ufanisi Isabellah Lumumba alisema ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kuwa ametunza mazingira.
Lumumba pia aliiomba serikali ya kaunti ya Kisii kuwa katika msitari wa mbele katika upanzi na uhifadhi wa mazingira,
Lumumba aliihimiza kuelimishwa kwa watoto kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira ili wanapokuwa wawe wanafahamu maana ya uhifadhi wa mazingira.
                                           Thanks by yard family

Comments

Popular posts from this blog

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal.

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries were on Wednesday charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal. Obure who was charged over crimes committed when he was a Minister of Finance in former President Daniel arap Moi’s government, was in the dock alongside former Transport and Communication Permanent Secretary Sammy Kyungu, former PS Ministry of Finance Joseph Magari and former PS for Internal Security and Provisional Administration Dave Mwangi. They have all denied abuse of office and conspiracy to commit economic crime charges, although Mwiraria and the Kamani’s who are represented by lawyer Ahmednassir Abdullahi were not in court/CFM NEWS Also charged alongside them were former Postmaster General Francis Chahonyo, former Finance Secretary Samuel Bundotich and David Onyonka who was in-charge of debt management in the Ministry of Finance at the time he is accused of committing economic crimes. David Mwiraria who...

MALLS ACROSS COUNTRY ON HIGH ALERT AFTER AL-QAEDA LINKED TERROR THREAT

A video purported to be by Somalia's al-Qaida-linked rebel group al-Shabab urged Muslims to attack shopping malls in the U.S., Canada, Britain and other Western countries. U.S. authorities said there was "no credible" evidence suggesting a U.S. mall attack was in the works. The threat by the al-Qaida affiliate came in the final minutes of a more than hourlong video released Saturday in which the extremists also warned Kenya of more attacks like the September 2013 assault on the Westgate Mall in Nairobi in which 67 people were killed. The masked narrator concluded by calling on Muslims to attack shopping malls, specifically naming the Mall of America in the Minneapolis suburb of Bloomington, as well as the West Edmonton Mall in Canada and the Westfield mall in Stratford, England. The authenticity of the video could not be immediately verified by The Associated Press. The FBI and Department of Homeland Security provided local law enforcement agencies and private sec...
kisii County News Thursday,June 18 2015 Father jailed for 30 years for killing son A signboard showing directions to Kisii law courts. A father was jailed for 30 years by the High Court in Kisii for killing his son. A man was jailed for 30 years by the High Court in Kisii after he was convicted of murdering his son. Kennedy Obara murdered his two and a half year old son, Hezbon Nyamongo by strangling him on April 11, 2013 at Nyaramba sub location in Gucha South, Kisii County. The court was told that Obara, who had a habit of beating his wife, had beaten her on the fateful night using a walking stick after which she fled to her parents at Suguta. She left behind her two sons who included the deceased and his seven-year-old brother. Kisii Resident Judge Ruth Sitati said that after carefully examining the evidence given by the prosecution and the cross examination, she concluded that it was Obara who killed the deceased. She said that in her considered view there was sufficient...