Skip to main content

Posts

Showing posts from May 31, 2015

YANAYOJIRI juni/06/2015

--Ni wakati wa kupokea habari za yard fm NA AGR FM lakini kwanza mkhutasari wake. ---Ni haki yetu kutengenezewa barabara wakaazi wa Nyaribari Masaba wasimama kidete ----Lazima gavana atueleze yale ametekeleza kimaendeleo kwa kaunti ya Nyamira mbunge wa Kitutu Masaba Timoty Bosire akariri ----Soko la Gesusu kupata sura mpya karibuni ---Wanahabari wa Kisii wajipata matatani tena kwa kutoa habari si halisi 1   wakaazi  wa eneo Bunge la Nyaribari Masaba, Kaunti ya Kisii waliandamana hiyo jana, kulalamikia  hali mbaya ya barabara ya kutoka makutano ya  Geteri  kuelekea soko la Geteri ambayo kwa sasa haipitiki. Waendeshaji Bodaboda waliojawa na gadhabu walilalamikia hali duni ya barabara hiyo ambayo kwa sasa haipitiki kamwe kufuatia mvua nyingi inaendelea kunyesha katika sehemu za Kisii. Vijana hao wakiongozwa na mwenyekiti wa Bodaboda wa eneo hilo Mong’eri Nyabicha walichukua hatua ya kupanda mgomba wa ndizi katika barabara hiyo na kutatiza usafiri wakidai kwamba kuliilima b

TAARIFA YA HABARI 06/04/2015

 -- karibu kwa taarifa zetu jioni/asubuhi hii  wakati wa kupokea habari za yard na AGR fm lakini kwanza tupate mkhutasari wake --Ni maisha yetu lazima tume ya TSC itujali maslahi  yetu walimu wa --masaba kazikazini wasimama kidete. --Msipofanya kazi vizuri zitawapatia pesa mwakilishi wa magenche awambia wanakandarasi --Kanisa zote zaombwa kushirikiana kupambana na madawa za kulevya kisii hujambo 1 Walimu kutoka wilaya ya Masaba kaskazni wameiomba tume ya kuwaajiri  walimu [TSC] kuwajali  wakati wa kuwahamisha  walimu hao hadi shule zingine. Akiongea hiyo jana katika  eneo la  Masaba kaskazini kaunti ya Nyamira  mwenyekiti wa walimu kutoka masaba Meshack Obonyo ameiomba tume ya kuwaajiri walimu [TSC] kuzingatia afya na masuala mengine ya walimu kabla ya kuwahamisha  hadi shule  zingine. Kulingana na Meshack walimu uhamishwa kuenda katika shule zingine ambazo ni mbali kutoka  sehemu wanakoishi   jambo ambalo amesema huwa ngumu kwa walimu hao kwani  kiwango cha pesa wananachoka

Mafuriko na vilio Dar

Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam WATU wanane wamefariki dunia kutokana na mafuriko ya mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam. Akitoa taarifa ya vifo hivyo Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema watu watano wametambuliwa na wengine watatu bado hawajatambulika na miili yao imehifadhiwa katika ya Hospitali ya Mwananyamala. Alisema Mei 6 mwaka huu, saa moja usiku maeneo ya Magomeni wilayani Kinondoni, mkazi wa Manzese, Shabani Idd (73), alisombwa na maji ya Mto Ng’ombe alipojaribu kuuvuka na mwili wake ulipatikana Mei 7 akiwa amefariki. “Kifo kingine kilitokea Mei 7, mwaka huu mnamo saa 6 mchana maeneo ya Mwananyamala Mbuyuni ambako Masumbuko Douglass (50) alianguka na kufariki dunia ghafla wakati akitoa maji yaliyoingia ndani kwake na uchunguzi wa awali unaonyesha alikuwa na kifafa hivyo wakati akihangaika kutoa maji ugonjwa huo ulimpata na kuanguka,” alisema Kova. Alisema Mei 6, mwaka huu mkazi wa Mvuruhana Pemba Mnazi,

Mafuriko yaua watatu Nairobi

Watu watatu wameaga dunia wakati mvua imenyesha usiku wa kuamkia leo kule Nairobi. Mvua nyingi imeonekana ikileta maafa na mafuriko hivi karibuni kuanzia Nairobi, narok na hata Pwani ya Kenya. Juma lililopita mvua pia ilionekana kuleta maafa katika jimbo la Texas nchini marekani. Kuna haja ya kulinda mazingira na kutafakari anga ili kuepukana na hali kama hii. Orina ontiri, AGR news.

30 mei 2015

Vidokezo --Mwanasiasa aapa kuendelea kuwasaidia watoto mayatima eneo bunge la kitutu masaba kaunti ya Nyamira  Nyamira --wazazi waombwa  kuchukua vyeti vya kuzaliwa  kutoka kwa ofisi ya kuwasajili  kwa kuwa viko tayari  kwa wanao. ---Msitumiwe na wanasiasa vijana kutoka eneo bunge la Kitutu masaba kaunti ya nyamira waambiwa na mbunge wao.   …………….. 1]  Mwanasiasa   Ogeto Swanya  kutoka eneo bunge la Kitutu Masaba ameapa kuendelea kuwasaidia mayatima wa eneo bunge hilo kupata elimu. Akiongea Ijumaa katika  hafla  ya mazishi ya mama  Mary Simeon kijiji cha Riamisiani wadi ya Gesima Ogeto alisema anataka kuinua kiwango cha masomo katika eneo bunge hilo. Aidha, aliwaomba wakazi wote kushirikiana  ili kuinua viwango vya masomo  kwa kuwa ndio itasaidia kupata viongozi wa kesho. Ogeto alisema kuwa atatembelea shule zote katika eneo hilo huku akiwatabua watoto mayatima. Kwa upande mwingine aliwaomba viongozi waliomamlakani kwa sasa kuwasaidia wananchi ili kuinua viwango v