Skip to main content

Mafuriko na vilio Dar

Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam

WATU wanane wamefariki dunia kutokana na mafuriko ya mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam.

Akitoa taarifa ya vifo hivyo Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema watu watano wametambuliwa na wengine watatu bado hawajatambulika na miili yao imehifadhiwa katika ya Hospitali ya Mwananyamala.
Alisema Mei 6 mwaka huu, saa moja usiku maeneo ya Magomeni wilayani Kinondoni, mkazi wa Manzese, Shabani Idd (73), alisombwa na maji ya Mto Ng’ombe alipojaribu kuuvuka na mwili wake ulipatikana Mei 7 akiwa amefariki.

“Kifo kingine kilitokea Mei 7, mwaka huu mnamo saa 6 mchana maeneo ya Mwananyamala Mbuyuni ambako Masumbuko Douglass (50) alianguka na kufariki dunia ghafla wakati akitoa maji yaliyoingia ndani kwake na uchunguzi wa awali unaonyesha alikuwa na kifafa hivyo wakati akihangaika kutoa maji ugonjwa huo ulimpata na kuanguka,” alisema Kova.
Alisema Mei 6, mwaka huu mkazi wa Mvuruhana Pemba Mnazi, Kigamboni, Rashidi Hassan (36), alizama katika mkondo wa maji unaoelekea baharini na mwili wake ulipatikana juzi ukiwa unaelea majini umbali wa mita 500 toka eneo alilozama.
“Kifo kingine kimetokea Mei 6 mwaka huu eneo la Yombo Makangarawe ambako mtoto, Gloria Mrema mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu alipotea baada ya watoto wenzake kumuacha wakati wakicheza kwa pamoja na juhudi za kumtafuta zilifanyika bila mafanikio hadi mwili wake ulipopatikana ukiwa unaelea majini katika Mto Mzinga akiwa tayari amepoteza maisha na mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Temeke,” alisema Kova.
Alisema kifo kingine kilitokea jana eneo la Kinondoni Mkwajuni baada ya mtu mmoja mwanaume jina lake halikufahamika anakadiriwa kuwa na umri kati miaka 40 au 45 alikutwa amefariki dunia na mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi.
“Pamoja na vifo hivyo kuripotiwa, pia mtu mmoja Mabula Moses (65) ambaye ni mkazi wa Vingunguti wilayani Ilala amevunjika mguu wake wa kulia chini ya goti baada yakuangukiwa na ukuta wa ghala la Fida Hussen lililopakana na nyumba yake na majeruhi amepelekwa katika Hospitali ya Amana,” alisema Kova.
Alisema katika Kata ya Mchikichini taarifa ya mafuriko inaonyesha nyumba takriban 70 zimefunikwa na maji hadi juu ya paa na wakazi wake tayari wamehama huku watu 35 wamejihifadhi Shule ya Sekondari Mchikichini.
“Kata ya Jangwani zipo nyumba takriban 100 zimefunikwa na maji hadi juu ya paa na watu 300 walihama mapema.
“Maeneo mengine yaliyoathirika zaidi kutokana na mvua hizo ni Keko, Changombe Maduka Mawili, Yombo Vituka, Vingunguti, Afrikana, Msasani Bonde la Mpunga, Jangwani, Manzese, Kigogo, Mburahati, Boko Basihaya na maeneo mengine taarifa hazijapokelewa,” alisema Kova.
Aliwataka wananchi wote kuchukua tahadhari hasa wale wanaoishi maeneo ambayo ni mikondo ya maji au watumiaji wa barabara zinazopitiwa na mikondo hiyo.

MTANZANIA lilitembelea baadhi ya maeneo ya jiji hilo na kujionea hali halisi ya mafuriko na kukuta sehemu nyingi zikiwa zimezungukwa na maji.
Pia mvua hizo zilisababisha zaidi ya kaya 80 katika kata za Wereweru, Masama, Rundugai na Mnadani wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kukosa makazi baada ya nyumba zao kusombwa na maji.

Mbali na kaya hizo kukosa makazi, pia mafuriko hayo yameharibu vibaya miundombinu mbalimbali ya barabara ikiwemo madaraja kusombwa na maji pamoja na miundombinu ya reli kuharibika ikiwa ni pamoja na hekari 450 za mazao mbalimbali kuchukuliwa na maji.

Akizungumzia athari za mafuriko hayo, Mkuu wa Wilaya ya Hai, Athony Mtaka, wakati akikabidhiwa msaada wa vifaa mbalimbali vya waathirika hao na Benki ya NMB, alisema mvua hizo zilizoanza kunyesha Mei 2, mwaka huu zilileta madhara makubwa kwa wananchi.

Kwa Mkoa wa Tanga, zaidi ya kaya 60 hazina mahali pa kuishi baada ya nyumba zao kuzingirwa na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Nyumba hizo zipo katika eneo la Magaoni, Donge na Mtaa wa Mabawa A zilizopo Kata ya Mabawa.

Naibu Meya wa Jiji la Tanga, Mzamili Shemdoe, alithibitisha kupokea taarifa za kuwepo kwa kaya zilizoathirika na mvua hizo.

Katika hatua nyingine, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema mvua hizo zitaendelea kwa muda wa siku 12 kuanzia leo.
Habari hii imeandaliwa na Tunu Nassor, Esther Mnyika, Johanes Respichius na Herieth Faustine wa Dar es Salaam na Upendo Mosha wa Kilimanjaro na Amina Omari wa Tanga.

Comments

Popular posts from this blog

ICC: Abasoeri na abaegereri komogorerana ekegambero ekenene kia ICC

Ekeombe kia obosoeri aaria chinsemo chia ICC nigo bamogorerana rituko ria rero ase okogenderera kobora gwa kirori P0727. Koreng'ana na obosoeri, kirori oyio noyobengencho enene. Korwa abakweegerera Ruto na Sang', nigo baangire kirori oyioo taganywa ekiagera babakoreire chimgaki na ebiro gose koegwa ribaga ria bene komoringooria orogendo rwaye oborori bwaye botarategererwa. Nigo ekageire buna kirori oyio nere oyo' omoerio. Ankio nigo ekegambero kerarwe ribaga ase ebiombe ebio bibere kogayana ogotaigwana okwo.

Dallas/Ft. Worth hit with up to 7 inches snow!

It’s a winter wonderland in Dallas/Ft. Worth! We were expecting the sleet and freezing rain last night but the snow was an added bonus! Between 3 and 7 inches dropped across the metroplex. Temps are expected to get up to around 37 which means some of ice and snow will melt but temps will drop below freezing tonight causing what melts to re-freeze-KRNB

Hey Men.....6 Ways Men are Destroying their Sperm

It’s not only women who suffer from infertility problems. Men are also the victim to fertility issues. The sperm plays an important role in fertilization. The lifestyle people lead today lead to the disintegration of the quality of the sperm and its production. Here are some issues that affect his sperm levels: Keeping their phones in the front trouser pockets All of us know the ill effects of radiation emitted from our phones and yet we choose to keep them in our trouser or jeans pockets. It’s not all talk but research that has proved that the radiation emitted from our phones kill the sperms in his pants. So if you are worried about fertility issues, remind your guy to keep his cellphone elsewhere. Excessive smoking Smoking is bad for the overall health. It even affects the sperm in a negative way. Smoking apart from reducing the  sperm count  also prevents it from moving around. Stress Stress affects all our bodily functions including the production o...