Skip to main content

Posts

Showing posts from June 7, 2015

Taarifa 06/11/2015

--Waziri wa fedha Henry Rotich asoma Bujeti ya mwaka wa 2015-2016 . --tunaomba serikali kuwatia mbaroni wakimbizi ghushi     asema mwenyekiti Nemuel Momanyi --ni haki yetu hatutarudisha sare za kazi        wafanyikazi wa nyamira wasimama kidete. --kamishena wa kisii chege mwangi kuzuru eneo la gesure hivi karibuni 1 Bajeti ya mwaka wa 2015-2016  imesomwa hii leo katika ukumbi wa bunge la kitaifa ikiwasilishwa na waziri wa fedha nchini Henry Rotich. Bajeti hiyo ya pesa taslimu shillingi trillion mbili itanufaisha baadhi ya sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya kutengeneza barabara kutengewa kiwango kikubwa cha  pesa. Hii ni mara ya pili bajeti kusomwa chini ya uongonzi wa serikali ya Jubilee huku wakenya wengi walikuwa wanatarajia bei ya bidhaa kushuka na hata masuala muhimu ikiwa suala la kuimarisha usalama nchini .  2Mwenyekiti wa wakimbizi wa ndani walioathirika kufuatia ghasia zilizozuka baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 katika kaunti za Nyamira na Kisii ameomba serikali kuu ku

Bwana Yesu Kristo hakufa Msalabani ili atimize Ndoto Yako

LUGHA MPYA: Mtazamo wa ulimwengu, nia ya kibinadamu na ya wasioamini zimeingia fikra za waumini wengi sana. Wapendwa wasomaji, wapi katika Agano Jipya  tunasoma kwamba Yesu au mitume wanawasisitiza waumini wazifuate ‘ndoto’ zao? Haipo! Wapi katika maandiko ya Biblia  waandishi wanatumia lugha ya ‘zifuate ndoto zako’? Haipo! Wapi Bwana Yesu alisema, “Nimekuja kuitumiza ndoto yangu.”? Haiwezekani! Siyo ndiyo? Yesu wala mitume wake hawakuitumia lugha hiyo au maneno haya! Wazo hili linapinga mafundisho ya neno la Mungu. Wazo hili linainua hamu yangu yenyewe au tamani yangu ya binafsi kuliko mapenzi ya Mungu kwa maisha yangu! Ni mafundisho ya hatari sana siku hizi. Bwana Yesu hakufa ili atimize ndoto yako bali mapenzi ya Mungu yatimizwe katika maisha yako. Watu, na hata wahubiri, wanasema, ‘Fuata ndoto zako!’ Lakini Yesu alisema, ‘Nifuate mimi’. Ikiwa utafuata ndoto zako, unajifurahisha mwenyewe tu. Lakini ikiwa utamfuata Yesu, atampendeza Yeye. Kama utafuata ndoto zako, basi unajit

Taarifa ya 06/11/2015

1]Mwenyekiti wa wakimbizi wa ndani walioathirika kufuatia ghasia zilizozuka baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 katika katika kaunti za Nyamira na Kisii ameomba serikali kuu kuwachukulia hatua kali ya kisheria wale wanajitambulisha kuwa wakimbizi ili kufadhiliwa na serikali. Akiongea siku ya Jumatano na waandishi wa habari katika uwanja wa michezo wa Gusii, mwenyekiti huyo Nemuel Momanyi alisema kuna baadhi ya watu ambao wanajitambulisha kuwa wakimbizi wa ndani ilhali hawakufurushwa kutoka popote ila ni mbinu ya kufadhiliwa na serikali ya kitaifa. Hii ni baada ya wakimbizi wa ndani 23,000 katika eneo la Gusii wanaostahili kufadhiliwa na serikali kusema kuwa hawajawahi pata msaada wowote kutoka kwa serikali hadi sasa.  Wakati huo huo mwenyekiti huyo alisema kuwa ni wakimbizi hao bandia wanaishi vizuri baada ya kupata pesa za bure kutoka kwa serikali ilihali wale halisi wanasumbuka. 2] Mbunge wa Homa-Bay Town Peter Kaluma ameziomba Serikali za ugatuzi pamoja na ile ya kitaifa kushirik

TAARIFA LEO 06/10/2015

Hizi ni habari zetu sikitayarishwa na Peter Onkoba na Brighton makori 10th  June 2015 1]Hafla ya kukusanya maoni kutoka kwa wakaazi wa Kisii ambayo ilifanyika jana Jumanne katika ukumbi wa Cultural Centre ilishuhudia watu wachache sana ambao walihudhuria kongamano hilo. Kampeni hiyo ambayo imekuwa ikiendelea kwa muda sasa kwenye kaunti mbali mbali kote nchini, iliweza kuhudhuriwa naye mwenyekiti wa pesa za maendeleo za maeneo bunge maarufu kama CDF, Elias Mbao pamoja na mbunge wa eneo bunge la Nyaribari Masaba  Elijah Moindi ambaye pia ni mwanachama wa kamati teule ya bunge inashughulikia pesa hizo za CDF ambaye pia anawakilisha kaunti mbili za eneo la Gusii; Kisii na Nyamira. Ukumbi huo ambao kwa kawaida hujaa pomoni kunapokuwa na hafla kama hizo, ulijazwa nusu, ambapo mwenyekiti Mbao alivilaumu vyombo vilivyowajibishwa kusambaza ujumbe huo kwa kutofanya kazi yao kikamilifu. Hata hivyo, wengi waliohudhuria kongamano hilo waliunga mkono kuwe na pesa hizo za maendeleo ya maneo

TAARIFA JUNI 8 2015

Ni wakati wa kupokea habari za yard na AGR fm lakini kwanza tupate mkhutasari wake --Naomba wasomi kutembelea shule za kisii kuwaeleza wanafunzi umuhimu wa masomo mbunge Elijah moindi akariri --Ni maisha na haki yetu kutengenezewa daraja wakaazi wa Gesima waambia serikali ya Nyamira. 1 Mbunge  wa eneo bunge la Nyaribari Masaba Kaunti ya Kisii Elijah Moindi amewaomba wasomi wote kutembelea shule zilizoko kaunti hiyo kuwaelezea wanafunzi umuhimu  wa mosomo kama njia moja ya kuwatia motisha wanafunzi katika masomo. Akizungumza siku ya Jumapili katika eneo bunge lake wakati alikuwa akitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imetekelezwa kupitia pesa za hazina ya ustawi maeneo bunge CDF  Mbunge huyo aliomba wasomi kutembea katika shule za msingi na za upili kuwaeleza wanafunzi maana ya masomo na kuwaelimisha wanafunzi kutia bidii wakiwa katika shule ili eneo la Kisii linawiri zaidi  kwa masomo. Mwakilishi huyo pia aliwaomba wakaazi wa eneo bunge lake kushirikiana na ofi

TAARIFA KAMILI KISII

-Ni wakati wa kupokea habari za yard fm na AGR FM, abagusii global radio lakini kwanza tupate mkhutasari wake. Naomba makanisa mjitolee tuombee nchi yetu -asema dakari Nyandoro -Mbunge wa  Nyaribari Masaba Elijah Moindi   asema shule zizawadiwe baada ya kufanya vyema katika  mitihani -Wakaazi wa kisii waombwa kumpa gavana ongwae mda kufanya maendeleo. -Wanaochimba barabara wakamatwe na kushtakiwa asema mbunge Timothy Bosire HABARI KAMILI: 1 Makanisa yote  yameombwa kuombea nchi ya Kenya ili kuwe na amani na kuzuia visa vya mashambulizi kuendelea kushuhudiwa nchini. Akiongea jana katika hafla ya kuchangisha fedha za ujenzi wa kanisa ya kiadventista ya Tindereti iliyoko eneo bunge la Borabu kaunti ya Nyamira daktari Yobesh Kambi aliomba wahumini wa makanisa mbalimbali kuendelea kuombea nchi ya Kenya ili amani iendelee kushuhudiwa. Wakati uo huo, daktari Nyandoro aliomba wakaazi kushirikiana pamoja kuleta maendeleo katika jamii ya mkisii haswa katika kaunti ya Nyamira.