Skip to main content

Taarifa ya 06/11/2015

1]Mwenyekiti wa wakimbizi wa ndani walioathirika kufuatia ghasia zilizozuka baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 katika katika kaunti za Nyamira na Kisii ameomba serikali kuu kuwachukulia hatua kali ya kisheria wale wanajitambulisha kuwa wakimbizi ili kufadhiliwa na serikali.

Akiongea siku ya Jumatano na waandishi wa habari katika uwanja wa michezo wa Gusii, mwenyekiti huyo Nemuel Momanyi alisema kuna baadhi ya watu ambao wanajitambulisha kuwa wakimbizi wa ndani ilhali hawakufurushwa kutoka popote ila ni mbinu ya kufadhiliwa na serikali ya kitaifa.
Hii ni baada ya wakimbizi wa ndani 23,000 katika eneo la Gusii wanaostahili kufadhiliwa na serikali kusema kuwa hawajawahi pata msaada wowote kutoka kwa serikali hadi sasa.
 Wakati huo huo mwenyekiti huyo alisema kuwa ni wakimbizi hao bandia wanaishi vizuri baada ya kupata pesa za bure kutoka kwa serikali ilihali wale halisi wanasumbuka.

2] Mbunge wa Homa-Bay Town Peter Kaluma ameziomba Serikali za ugatuzi pamoja na ile ya kitaifa kushirikiana pamoja na kufanya maendeleo katika sehemu zote nchini.

Akizungumza siku ya Jumanne katika ukumbi wa Gusii Cultural Hall mjini Kisii kwenye hafla ya kusanya maoni ya wanchi kuhusu pesa za hazina ustawi maeneo bunge (CDF), Mbunge Kaluma alisema sharti Serikali za ugatuzi na ile ya Kitaifa zishirikiane ili kufanya maendeleo zaidi katika sehemu zote za nchi.
Matamshi ya mbunge huyo yaliungwa mkono na Mbunge wa Nyaribari Masaba Elijah Moindi ambaye alisema kuwa Serikali zote zikishirikiana pamoja maendeleo yatafanyika zaidi katika sehemu za mashinani huku akiomba viongonzi wote kuweka siasa kando na kutilia maanani maendeleo. 
hospitalli moja. [Picha/ Money-kisumunews.com]]

3]Mwanasiasa mmoja kutoka eneo bunge la Nyaribari Chache katika kaunti ya Kisii Rael Otundo amesema pesa ambazo serikali ya kaunti ya Kisii ilitenga kuwanunulia wananchi kadi za matibabu ya NHIF zinastahili kutumika kununua dawa katika hospitali moja ili kuwafaidi Wananchi wote.
Akizungumza siku ya Jumanne katika hafla ya mazishi katika kijiji cha Nyanguru, kaunti ya Kisii, mwanasiasa huyo alisema ununuzi wa kadi hizo za NHIF hautasaidia maanake si kila mtu atafaidi.
Hii ni baada ya gharama ya kuilipia kadi hiyo kupanda kutoka shillingi 160 hadi shillingi 500 kwa kila mwezi, ambazo serikali ya kaunti ya Kisii haitaweza kulipa kila mwaka maana zitakuwa nyingi na kuigharimu serikali kutumia pesa nyingi zaidi.

4]Mbunge wa Nyaribari Masaba, Kaunti ya Kisii Elijah Moindi amewaomba wakaazi wa kaunti hiyo kuchukua hatua kwa Wabunge wanaoshukiwa kutumia vibaya pesa za hazina ya CDF.

Akiongea siku ya Jumanne katika ukumbi wa Cultural Hall mjini Kisii wakati wa kukusanya maoni ya wananchi kuhusu hazina ya CDF kusalia kuwa katika Serikali ya Kitaifa au iwe chini ya Serikali za kaunti, Mbunge Moindi aliomba wakaazi hao kuwashtaki  Wabunge ambao wanatumia pesa za maendeleo ya CDF vibaya ikiwa wana ushahidi wa kutosha.
Wakati uo huo, Mbunge huyo aliomba wananchi kuunga mkono maendeleo yanayofanywa katika maeneo bunge yao kupitia pesa hizo za CDF ili maendeo yainuke zaidi katika Kaunti ya Kisii.
Kwa upande mwingine viongozi waliohudhuria hafla hiyo waliunga mkono pesa hizo kubaki kwa Serikali ya kitaifa na ziongezwe zaidi kutoka asilimia 2.5 hadi asilimia 10.

5]Mwili wa mwanaume wa miaka ishirini na tisa ulipatikana ukiwa kando mwa mto Iyenga katika wadi ya Gesusu Kaunti ya Kisii Jumanne asubuhi.

Mwanamme huyo alitoweka kutoka kwake kwa njia isiyo eleweka siku tatu zilizopita, na kisha mwili wake kupatikana ukiwa kando mwa mto huo ulio eneo la Raganga, katika wadi ya Gesusu.
Inasemekana mwenda zake alitoka kwake na wenziye, lakini hakuregea jioni, huku mke wake akiripoti kwa ndugu zake na wakaanza shughli za kumsaka siku iliyofuata, na juhudi zao zilikumbwa na changamoto kwani hakuwa na simu.
Walipiga ripoti kwa chifu wa eneo hilo Bw Machogo Nyauma, ambaye pia alichukua hatua siku ya tatu kumtafuta bila mafanikio na kisha baadaye, mnamo saa tatu asubuhi wapita njia wakamtambua akiwa amefariki.
Mwili wake ulipelekwa katika chumba cha kuifadhi maiti cha Gucha Keroka, katika Kaunti ya Kisii, huku hicho kikiendelea kufanyiwa uchunguzi.
Chifu huyo aidha alisema amewaarifu polisi ambao wameanza kuchunguza kisa hicho ambacho ni cha aina yake

Na katika Michezo

Timu ya Shabana inayoshiriki ligi ya FKF inaendelea na mazoezi katika uga unaokarabatiwa wa Gusii, ili kujiandaa kwa mechi yao ya siku ya Jumapili dhidi ya FC Talanta.

Mechi hiyo ambayo itachezewa katika uwanja wa Awendo Green mjini Awendo, itashuhudia vijana hao wa Kisii wakikwaruzana na vijana wa Talanta, kwenye mechi hiyo inayotarajiwa kuwa ngumu.
Shabana, chini ya ukufunzi wa James Nandwa inashikilia nafasi ya kumi na moja kwenye jedwali la ligi ya FKF, na itakuwa ikijiandaa kuhakikisha matokeo yao yanaimarika.
Aidha, timu hiyo imekumbwa na habari mbaya, kufuatia fununu kwamba mchezaji wa kiungo cha kati Sunday Mutuku atahama klabu hiyo baada ya kandarasi yake kukamillika.
Mutuku, ambaye ameisaidia sana timu hiyo ameonyesha nia ya kuhama timu hiyo, huku fununu zikionyesha kuwa huenda akajiunga na Muhoroni Youth ingawaje habari hizo hazijadhibitishwa.
Kocha Nandwa amesema hatima ya Mutuku itajulikana pindi tu akapozungumza naye.
Halikadhalika, kocha huyo amesema kwamba bado timu hiyo ina nafasi nzuri ya kutua ubingwa wa ligi ya FKF, ikiwa watajizatiti na kutia bidii mara dufu

Hizi ndizo habari zetu zikitanyarishwa kwenu na Brighton Makori na kusomwa na Orina Ontiri

Comments

Popular posts from this blog

Al-Shabaab gunmen take hostages after deadly Kenya university attack

Militants claim to be holding Christian hostages after dawn raid on hostels in which they opened fire on students and security guards, killing at least 15 people Masked gunmen from Somalia’s al-Shabaab movement claim to be holding an unknown number of Kenyan Christians hostage after a dawn raid on a university compound that left at least 15 people dead. The attackers stormed into the university shortly after 5am in the town of Garissa, about 90 miles from the volatile border with Somalia. Kenya’s national disaster operations centre said 280 of the university’s 815 students were accounted for but did not say how many it believed to be still inside. The gunmen were in one of four residential buildings, the interior ministry said. InteriorCNG Ministry          ✔   @InteriorKE Follow #GarissaAttack Update: Of the four hostels, 3 have been evacuated. The attackers have been cornered in one hostel & the operations continue. 3:05 AM - 2 Apr 2015 Arnolda Shiundu, a spoke

What you need to Know about EDV 2023 (US Green card lottery program)

Success Africa ON AGR with Sylvester Oluoch hosted by Arphaxad Nyabuto