Skip to main content

Taarifa 06/11/2015


--Waziri wa fedha Henry Rotich asoma Bujeti ya mwaka wa 2015-2016 .
--tunaomba serikali kuwatia mbaroni wakimbizi ghushi     asema mwenyekiti Nemuel Momanyi
--ni haki yetu hatutarudisha sare za kazi        wafanyikazi wa nyamira wasimama kidete.
--kamishena wa kisii chege mwangi kuzuru eneo la gesure hivi karibuni

1 Bajeti ya mwaka wa 2015-2016  imesomwa hii leo katika ukumbi wa bunge la kitaifa ikiwasilishwa na waziri wa fedha nchini Henry Rotich.
Bajeti hiyo ya pesa taslimu shillingi trillion mbili itanufaisha baadhi ya sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya kutengeneza barabara kutengewa kiwango kikubwa cha  pesa.
Hii ni mara ya pili bajeti kusomwa chini ya uongonzi wa serikali ya Jubilee huku wakenya wengi walikuwa wanatarajia bei ya bidhaa kushuka na hata masuala muhimu ikiwa suala la kuimarisha usalama nchini .

 2Mwenyekiti wa wakimbizi wa ndani walioathirika kufuatia ghasia zilizozuka baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 katika kaunti za Nyamira na Kisii ameomba serikali kuu kuwachukulia hatua kali ya kisheria wale wanajitambulisha kuwa wakimbizi ili kufadhiliwa na serikali.
Akiongea hiyo  jana na  waandishi wa habari katika uwanja wa michezo wa Gusii, mwenyekiti huyo Nemuel Momanyi alisema kuna baadhi ya watu ambao wanajitambulisha kuwa wakimbizi wa ndani ilhali hawakufurushwa kutoka popote ila ni mbinu ya kufadhiliwa na serikali ya kitaifa.
Hii ni baada ya wakimbizi wa ndani 23,000 katika eneo la Gusii wanaostahili kufadhiliwa na serikali kusema kuwa hawajawahi pata msaada wowote kutoka kwa serikali hadi sasa.
Wakati huo huo mwenyekiti huyo alisema kuwa ni wakimbizi hao bandia wanaishi vizuri baada ya kupata pesa za bure kutoka kwa serikali ilihali wale halisi wananasumbuka.
3 Mwathiriwa mmoja wa ghazia za uchaguzi wa mwaka wa 2007-2008 ameiomba serikali kumsaidia ili kujiendeleza kimaisha.
Akiongea na Waandishi wa habari hiyo jana katika hafla ya wakimbizi wanaotafuta haki ya kusaidiwa na Serikali katika uwanja wa Gusii, mwathiriwa Simeon Atandi Monyancha kutoka Bomorenda, eneo Bunge la Bonchari katika Kaunti Ya Kisii alielezea shida alizokumbana nazo katika mwaka wa 2007 wakati alikatwa mikono yake wakati wa ghazia za uchaguzi wa 2007-2008 katika sehemu ya Sotik.
Monyancha aliyekuwa na huzuni mwingi akiyasema aliyokumbana nayo wakati huo kwa sasa anaiomba Serikali kumsaidia kuweza kujipatia mapato ya kila siku.
Monyancha ambaye ni baba ya watoto sita na wake wawili, ilhali mkewe wa kwanza aliaga, alisema kuwa ana kibarua kigumu ya kulisha familia yake kwani hana lolote afanyalo kwa kukosa mikono yake miwili.
Monyancha alisema kuwa alikuwa akifanya kazi ya kuchuna majani chai alipokumbana na kisa hicho kilichomwacha bila mikono kwani alikatwa mikono na wenye walikuwa na maoni tofauti ya  kisiasa.
4Askari wa Kaunti ya Nyamira waliosimamishwa kazi wamelipinga ombi la Serikali ya Kaunti hiyo kuwahitaji kuzirudisha sare zao za kazi walizopewa hapo mbeleni.
Wakizungumza na Wandishi wa habari hiyo  jana katika mji wa Nyamira, wafanyikazi hao sasa wanataka haki itendeke kwa kupata suluhu mwafaka unaozingira kesi yao.
Mkuu wa Idara ya fedha katika Kaunti ya Nyamira John Omanwa amekanusha madai hayo ya kusema wanakandarasi walioajiriwa na Serikali ya kaunti hiyo ya Nyamira wamefutwa kazi ila wamesimamishwa kazi kufuatia wakati wao waliopatiwa kufanya kazi kama wanakandarasi kufika mwisho.
Aidha, Omanwa alisema watu huajiriwa katika kaunti hiyo kwa muda kati ya miezi mitatu hadi sita na watu hao pia kutafute ajira upya kufuatia sheria za Serikali ya kaunti hiyo.

Askari hao hata hivyo wamesimama kidete kwa kusema hawatarudisha sare zao ila kutendewa haki kama wakaazi wa kaunti hiyo.

5 Kamishena wa kaunti ya Kisii Chege Mwangi amewahakikishia wakaazi wa kata ndogo ya Gesure wilayani Sameta kaunti ya Kisii kuwa atazuru katika sehemu hizo kutafuta suluhu la kulalamikia kuajiriwa kwa naibu chifu wa eneo hilo ambaye anasemekana hakuajiriwa kwa njia ya haki ila ni kufuata ukoo wa nyumba Fulani.
Alizungumza afisini mwake hiyo jana kamishena Chege Mwangi alisema atazuru sehemu hizo hivi karibuni kutatua malalamishi ya wakaazi wa eneo hilo .
Hii ni baada ya yakaazi wa eneo hilo la Gesure kuandamana hadi ofisi yake hiyo jana wakiongozwa na David Ogega wakilalamikia kuajiriwa kwa naibu chifu wa lokesheni hiyo ya Gesure huku wakisema ni ufisadi na anatoka ukoo mmoja na chifu wa eneo hilo wakisema ni ufisadi kwa wakaazi wengine.
Sasa ni rasmi kuwa kamishena amesikia kilio chao na kuwahakikishia wakaazi hao kuwa atazuru sehemu hizo ili kusuluhisha mambo hayo.

Habari ambazo zimeandaliwa na Denis zadock  na Brighton makori

Comments

Popular posts from this blog

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal.

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries were on Wednesday charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal. Obure who was charged over crimes committed when he was a Minister of Finance in former President Daniel arap Moi’s government, was in the dock alongside former Transport and Communication Permanent Secretary Sammy Kyungu, former PS Ministry of Finance Joseph Magari and former PS for Internal Security and Provisional Administration Dave Mwangi. They have all denied abuse of office and conspiracy to commit economic crime charges, although Mwiraria and the Kamani’s who are represented by lawyer Ahmednassir Abdullahi were not in court/CFM NEWS Also charged alongside them were former Postmaster General Francis Chahonyo, former Finance Secretary Samuel Bundotich and David Onyonka who was in-charge of debt management in the Ministry of Finance at the time he is accused of committing economic crimes. David Mwiraria who...

MALLS ACROSS COUNTRY ON HIGH ALERT AFTER AL-QAEDA LINKED TERROR THREAT

A video purported to be by Somalia's al-Qaida-linked rebel group al-Shabab urged Muslims to attack shopping malls in the U.S., Canada, Britain and other Western countries. U.S. authorities said there was "no credible" evidence suggesting a U.S. mall attack was in the works. The threat by the al-Qaida affiliate came in the final minutes of a more than hourlong video released Saturday in which the extremists also warned Kenya of more attacks like the September 2013 assault on the Westgate Mall in Nairobi in which 67 people were killed. The masked narrator concluded by calling on Muslims to attack shopping malls, specifically naming the Mall of America in the Minneapolis suburb of Bloomington, as well as the West Edmonton Mall in Canada and the Westfield mall in Stratford, England. The authenticity of the video could not be immediately verified by The Associated Press. The FBI and Department of Homeland Security provided local law enforcement agencies and private sec...
kisii County News Thursday,June 18 2015 Father jailed for 30 years for killing son A signboard showing directions to Kisii law courts. A father was jailed for 30 years by the High Court in Kisii for killing his son. A man was jailed for 30 years by the High Court in Kisii after he was convicted of murdering his son. Kennedy Obara murdered his two and a half year old son, Hezbon Nyamongo by strangling him on April 11, 2013 at Nyaramba sub location in Gucha South, Kisii County. The court was told that Obara, who had a habit of beating his wife, had beaten her on the fateful night using a walking stick after which she fled to her parents at Suguta. She left behind her two sons who included the deceased and his seven-year-old brother. Kisii Resident Judge Ruth Sitati said that after carefully examining the evidence given by the prosecution and the cross examination, she concluded that it was Obara who killed the deceased. She said that in her considered view there was sufficient...