Skip to main content

TAARIFA LEO 06/10/2015

Hizi ni habari zetu sikitayarishwa na Peter Onkoba na Brighton makori 10th  June 2015

1]Hafla ya kukusanya maoni kutoka kwa wakaazi wa Kisii ambayo ilifanyika jana Jumanne katika ukumbi wa Cultural Centre ilishuhudia watu wachache sana ambao walihudhuria kongamano hilo.

Kampeni hiyo ambayo imekuwa ikiendelea kwa muda sasa kwenye kaunti mbali mbali kote nchini, iliweza kuhudhuriwa naye mwenyekiti wa pesa za maendeleo za maeneo bunge maarufu kama CDF, Elias Mbao pamoja na mbunge wa eneo bunge la Nyaribari Masaba  Elijah Moindi ambaye pia ni mwanachama wa kamati teule ya bunge inashughulikia pesa hizo za CDF ambaye pia anawakilisha kaunti mbili za eneo la Gusii; Kisii na Nyamira.

Ukumbi huo ambao kwa kawaida hujaa pomoni kunapokuwa na hafla kama hizo, ulijazwa nusu, ambapo mwenyekiti Mbao alivilaumu vyombo vilivyowajibishwa kusambaza ujumbe huo kwa kutofanya kazi yao kikamilifu.

Hata hivyo, wengi waliohudhuria kongamano hilo waliunga mkono kuwe na pesa hizo za maendeleo ya maneo bunge, ila wakapendekeza kubadilishwe watu na wasimamizi ambao wanadaiwa kuwa na uhusiano na wabunge wa maeneo ya uwakilishi.

Hafla hiyo ya kukusanya maoni imekuwa ikikusanya maoni kutoka kwa kaunti tatu katika kila kikao, ambapo hafla ya leo iliweza kuwakutanisha wakaazi wa kaunti za Kisii, Nyamira pamoja na kaunti ya Migori.

 2]Senate wa kaunti ya Nyamira amemtaka gavana wa kaunti hiyo kuhakikisha wafanyakazi wa vibarua wanalipwa pesa zao.

Senata huyo pia amewataka wafanyikazi hao kupewa kipaumbele katika kazi ambazo zimetangazwa na kaunti hiyo.

Akiongea na waandishi wa habari katika mji wa Nyamira siku ya Jumatatu, Seneta Okong’o Mong’are alishangazwa na swala hilo la kaunti hiyo kutowalipa wafanyakazi hao wa vibarua.

Alisema kuwa kuna pesa zilizotengwa kushughulikia malipo ya wahudumu wote wa kaunti ambao hufanya kazi katika vitengo mbali mbali katika kaunti hiyo.

Mong’are alimtaka gavana wa kaunti ya hiyo, John Nyagarama kuwajibikia maswala yanayomlenga.

Alimtaka gavana kushughulikia swala hilo liloripotiwa katika vyombo vya habari kuhusiana na vibarua ambao wanahudumu katika hospitali ya Nyamira level five ambao wamekuwa wakilalamikia kutolipwa hela zao kwa muda sasa.

Seneta huyo amekuwa mkosoaji mkubwa wa gavana wa kaunti hiyo yake kwa siku za hivi karibuni.

3Mbunge wa Homabay Town amewataka viongozi wote kutoka eneo pana la Nyanza Kusini ikiwemo Kisii kuunga mkono pesa za maendeleo ya maeneo bunge CDF, ili zibaki katika mikono ya wabunge.

Akiongea hiyo jana Jumanne  kwenye hafla ya kukusanya maoni kutoka kwa wakaazi wa kaunti za Kisii, Migori na Nyamira ambayo ilifanyiwa kwenye ukumbi wa umma wa Cultural Centre, Kaluma alisisitiza umuhimu wa pesa hizo ambazo alisema kuwa zimesaidia pakubwa kwa kuinua maendeleo ya maeneo ya mashinani.

Aliahidi kupigana hadi mwisho kuhakikisha pesa hizo zinabaki chini ya mamlaka ya wabunge, na kuona kuwa zinasimamiwa vizuri na pia kudokeza kuwa atasimamia mswada ambao utahakikisha kuwa matapeli ambao wamekuwa wakiwekwa na viongozi flani kusimamia pesa hizo wanaondolewa ili kulisafisha jina la usimamizi wa pesa hizo.

Pesa za maendeleo ya maeneo bunge zimekuwa na mzozo kati ya maseneta na magavana, huku wengi wa wananchi na viongozi wakitaka sheria maalumu kuwekwa ili kutoa uangalizi na usimamizi ulio wazi wa fedha hizo ambazo licha ya kufanya maendeleo katika mashinani, zimelaumiwa kwa kutoa mwanya kwa wabunge wengi kuwa wafisadi na kuwaajiri jamaa zao kusimamia miradi inayofadhiliwa na hela hizo.

Na katika Michezo

4Katibu mkuu wa michezo ya riadha katika viwango vya shule za msingi katika eneo la ziwa kuu Ben Ochieng’, amesema kuwa na imani wataibuka na ushindi mkubwa katika mashindano ambayo yalimalizika juzi  Jumatatu katika chuo cha Kisii.

Ochieng’ alikuwa akitoa hutuba yake ya kufunga mashindano hayo yaliyozikutanisha shule zaidi ya 30  za msingi kutoka kaunti za Migori, Homabay, Siaya, Kisumu, Nyamira pamoja na mwenyeji kaunti ya Kisii, ambapo hakuficha furaha yake kufuatia hali njema ya anga ambayo iliwapa nafasi mwafaka ya kufanikisha mashindano hayo bila shida.

Hata hivyo, katibu huyo alionyesha wasiwasi wake kwa wapinzani kutoka maeneo ya Bonde la Ufa ambalo alisema limekuwa mpinzani mkubwa, na kuwataka washiriki wote kuendelea kujiandaa mapema ili kuboresha matokeo hayo kufikia wiki ijayo tarehe 12 kutakapofanywa mashindano ya kitaifa.
Ochieng’ hakusita kuwaomba wanafunzi walioteuliwa kutumia faida ya kuwa wenyeji wa mashindano hayo kwa kuibuka na ushindi mnono.

Bado mashindano hayo hayajaamuliwa ni wapi hasa yataandaliwa kati ya uga wa michezo wa Gusii na ule wa chuo Kikuu cha Kisii, lakini Ochieng’ aliweza kudokeza kwamba huenda wakatumia uga wa Gusii kufuatia gavana wa kaunti hiyo kusema kuwa Chuo cha Kisii huenda kuwe na hafla nyingine.Mashindano hayo yataanza tena hapo kesho yakijumuisha kaunti zote.

5]Mwanafunzi wa miaka 11 alishangaza watazamaji waliojumuika katika uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Kisii siku ya Jumatatu baada ya kumenyana na zaidi ya wapinzani 50 kwenye mbio za mita 10,000 na kuibuka nambari tatu.

Mwanafunzi huyo alifuzu kuingia katika kikosi kitakachowakilisha eneo la ziwa kuu kwenye michuano ya riadha ya kitaifa ambayo itafanyika wiki ijayo.

Mwanafunzi huyo, Jane Ghati kutoka shule ya msingi ya Nyabikongori katika Kaunti ya Migori, alipata upinzani mkubwa kutoka kwa wanafunzi wenzake ambao walionekana kuwa na miili mikubwa na kuwa na misuli iliyotutumka lakini mtoto huyo hakushtushwa na wenzake hadi ilipofika mzunguko wa mwisho alitoka nambari ya kama kumi na tano ambapo aliwapita wanariadha waliokuwa mbele yake na kuridhika na nambari tatu.

Akiongea nawatangazaji wetu  baada ya kukamilisha shindano hilo, Ghati alionyesha furaha kubwa kwa kuteuliwa kuwakilisha eneo la Nyanza na kusema kuwa atajitahidi ili kufanya vizuri zaidi na kushinda wenzake katika kitengo hicho.

Mwenyekiti wa riadha kutoka kwenye kaunti anakotokea mwanafunzi huyo John Samwa, alisikitikia ukosefu wa msaada wa kifedha kutoka kwenye kaunti yao ya Migori, hali ambayo alitaja kuwa chanzo cha kuwasafirisha wanafunzi wachache kuwakilisha kaunti hiyo katika mashindano hayo.

Lakini mwenyekiti huyo hata hivyo alionyesha moyo wa kumpa motisha mwanafunzi Ghati kutimiza ndoto yake ya kuafikia mafanikio kwenye mbio hizo za mita 10,000.

                                           Thanks by Yard Family

Comments

Popular posts from this blog

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal.

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries were on Wednesday charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal. Obure who was charged over crimes committed when he was a Minister of Finance in former President Daniel arap Moi’s government, was in the dock alongside former Transport and Communication Permanent Secretary Sammy Kyungu, former PS Ministry of Finance Joseph Magari and former PS for Internal Security and Provisional Administration Dave Mwangi. They have all denied abuse of office and conspiracy to commit economic crime charges, although Mwiraria and the Kamani’s who are represented by lawyer Ahmednassir Abdullahi were not in court/CFM NEWS Also charged alongside them were former Postmaster General Francis Chahonyo, former Finance Secretary Samuel Bundotich and David Onyonka who was in-charge of debt management in the Ministry of Finance at the time he is accused of committing economic crimes. David Mwiraria who...

MALLS ACROSS COUNTRY ON HIGH ALERT AFTER AL-QAEDA LINKED TERROR THREAT

A video purported to be by Somalia's al-Qaida-linked rebel group al-Shabab urged Muslims to attack shopping malls in the U.S., Canada, Britain and other Western countries. U.S. authorities said there was "no credible" evidence suggesting a U.S. mall attack was in the works. The threat by the al-Qaida affiliate came in the final minutes of a more than hourlong video released Saturday in which the extremists also warned Kenya of more attacks like the September 2013 assault on the Westgate Mall in Nairobi in which 67 people were killed. The masked narrator concluded by calling on Muslims to attack shopping malls, specifically naming the Mall of America in the Minneapolis suburb of Bloomington, as well as the West Edmonton Mall in Canada and the Westfield mall in Stratford, England. The authenticity of the video could not be immediately verified by The Associated Press. The FBI and Department of Homeland Security provided local law enforcement agencies and private sec...
kisii County News Thursday,June 18 2015 Father jailed for 30 years for killing son A signboard showing directions to Kisii law courts. A father was jailed for 30 years by the High Court in Kisii for killing his son. A man was jailed for 30 years by the High Court in Kisii after he was convicted of murdering his son. Kennedy Obara murdered his two and a half year old son, Hezbon Nyamongo by strangling him on April 11, 2013 at Nyaramba sub location in Gucha South, Kisii County. The court was told that Obara, who had a habit of beating his wife, had beaten her on the fateful night using a walking stick after which she fled to her parents at Suguta. She left behind her two sons who included the deceased and his seven-year-old brother. Kisii Resident Judge Ruth Sitati said that after carefully examining the evidence given by the prosecution and the cross examination, she concluded that it was Obara who killed the deceased. She said that in her considered view there was sufficient...