Skip to main content

TAARIFA JUNI 8 2015

Ni wakati wa kupokea habari za yard na AGR fm lakini kwanza tupate mkhutasari wake
--Naomba wasomi kutembelea shule za kisii kuwaeleza wanafunzi umuhimu wa masomo mbunge Elijah moindi akariri
--Ni maisha na haki yetu kutengenezewa daraja wakaazi wa Gesima waambia serikali ya Nyamira.
1 Mbunge wa eneo bunge la Nyaribari Masaba Kaunti ya Kisii Elijah Moindi amewaomba wasomi wote kutembelea shule zilizoko kaunti hiyo kuwaelezea wanafunzi umuhimu  wa mosomo kama njia moja ya kuwatia motisha wanafunzi katika masomo.
Akizungumza siku ya Jumapili katika eneo bunge lake wakati alikuwa akitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imetekelezwa kupitia pesa za hazina ya ustawi maeneo bunge CDF  Mbunge huyo aliomba wasomi kutembea katika shule za msingi na za upili kuwaeleza wanafunzi maana ya masomo na kuwaelimisha wanafunzi kutia bidii wakiwa katika shule ili eneo la Kisii linawiri zaidi  kwa masomo.
Mwakilishi huyo pia aliwaomba wakaazi wa eneo bunge lake kushirikiana na ofisi ya hazina ya CDF ili maendeleo yafanyike zaidi kwa kueleza nini wanakihitaji wafanyiwe katika bunge hilo

2 Wakaazi wa wadi ya Gesima kaunti ya Nyamira wameofya maisha yao kutokana  na kuaribika kwa daraja lililoko katika barabara ya kutoka Nyamokono kuelekea Riakworo na maji kupita juu ya daraja hilo na watu kushindwa kupita.
Wakiongea na wanahabari hii leo asubuhi katika eneo hilo la Nyamokono ambapo daraja hilo liko wakaazi hao wakiongozwa na aliyekuwa diwani wa eneo la Gesima Julius Nyachio walisema wameofya maisha yao kwa kushindwa kupita katika daraja hilo ambalo maji yanapita juu na kuomba serikali ya kaunti ya Nyamira kutengeneza daraja hilo kabla maisha ya watu kupotea .
Daraja hilo ambalo hutumiwa na watu wengi zaidi limewazuia wakaazi wa eneo hilo kupita mpaka wanatumia njia ingine badala ambayo iko refu zaidi na wengine ambao ni wafanyikazi hujelewa kufika kwa kazi zao na haswa walimu pamoja na watoto wa shule.

3 Maafisa wa Trafiki pamoja na Askari wa Kaunti ya Kisii wametwikwa lawama kufuatia hali isiyokuwa ya kawaida iliyoshuhudiwa katika barabara zote za kuingilia na za kutoka katika mji wa Kisii.
Wakiongea na kituo hiki  baadhi ya wakaazi na wahudumu wa matatu ambao walikuwa wamekwama kwenye msongamano wa magari kwa zaidi ya saa mbili, waliwashtumu Maafisa hao kwa uzembe wanaposhughulikia masuala yanayomlenga mwananchi.
Charles Maina, dereva wa kampuni ya magari ya Mbukinya Travellers aligadhabishwa na utepetevu ulionyeshwa na Askari wa Kaunti hiyo akisema kuwa walikosa kuonyesha uwajibikaji wa kikazi na kuitaka Wizara ya Mipango na Uratibishaji wa mji kuwafundisha jinsi ya kuelekeza magari ili kupunguza msongamano wa magari ambayo imekuwa kero sana kwa wakaazi wa eneo hilo.
Kwa upande wake Jonhstone Mokua ambaye ni mwenyekiti wa Ziwani Matatu Sacco alionyesha kutoridhika kwake kuhusiana na msongamano huo ulioshuhudiwa siku ya Alhamisi ambapo aliwalaumu Mafisaa hao na kudai kuwa walikuwa wanapendea baadhi ya magari ya binafsi hasa wafanyakazi wa kaunti ambao walikuwa wanaruhusiwa kutumia njia mbadala ya RAM hospital ambayo ilichangia msongamano zaidi.

4Bunge la Kaunti ya Nyamira imetenga Sh10 milioni kwa ununuzi wa mitambo ya kurekodi maneno yanayojadiliwa katika bunge hilo, meza za kisasa na viti vya bunge hilo.
Pesa hizo zilitengwa hapo mbeleni kwa ujenzi wa nyumba ya kifahari ya Spika wa Kaunti hiyo pamoja na mkahawa wa bunge hilo, lakini zikabadilishwa kununua bidhaa hivyo muhimu katika bunge hilo kufuatia mswada uliopelekwa bungeni na Mwakilishi wa walio wengi katika bunge hilo Raban Masira na ukapitishwa.
Spika wa bunge hilo Joash Nyamoko aliuunga mkono uamuzi huo na kukubali pesa hizo kutumika kwa kununua mitambo ya kurekodi yale yanayojadiliwa katika bunge hilo.
Wawakilishi wengi waliounga mkono mswada huo na kusema yale wanahitaji katika kaunti ya Nyamira ni maendeleo bali sio kusafiri kama malkia au kuwa na makao ya kifahari.
Sasa ni rasmi kuwa pesa hizo zitatumika kununua mitamnbo katika bunge hilo ambayo itakuwa na manufaa zaidi kwa Wawakilishi hata kwa wakaazi wa kaunti hiyo kuyajua yale hua yanajadiliwa katika bunge hilo kama kumbusho kwa siku za usoni.


Na katika Michezo        Kaunti ya Kisii iliibuka na ushindi katika mashindano ya riadha kwenye ubingwa wa shule za msingi ambayo yalianza siku ya Jumapili na kukamilika hapo jana Jumatatu.

Mashindano hayo ambayo yaliandaliwa kwenye uga wa chuo cha Kisii, yalijumuisha kaunti sita kutoka mkoa wa Nyanza, yaliweza kushuhudia kuteuliwa timu ambayo itawakilisha eneo la Ziwa Kuu (Lake Region) katika mashindano ya Kitaifa ya riadha ya shule za msingi ambayo yatafanyika katika uga wa michezo wa Gusii Green.

Akiongea na  Yard radio pamoja na AGR, mkurugenzi wa elimu katika kaunti ya Kisii ambaye alikuwa mmoja wa maafisa waandalizi wa michezo hiyo, Bwa Richard Chepkawai alisema kuwa wanalenga kuimarisha michezo yote ya riadha katika kaunti ya Kisii na kudokeza kuwa watahakikisha kuwa wanaboresha matokeo yao zaidi ya jinsi wafanya leo.
Mashindano hayo yalijumuisha shule kutoka kaunti za maeneo Nyanza zikiwemo Migori, Homabay, Siaya, Kisumu, Nyamira pamoja na Kisii, ambao walikuwa wenyeji wa mashindano hayo ambapo vitengo mbali mbali vilishindaniwa kama vile mita elfu 10, mita 400 kupokezana vijiti miongoni mwa mashindano mengine.

imetayarishwa na Denis zadock

Comments

Popular posts from this blog

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal.

Kisii Senator Chris Obure and three former Permanent Secretaries were on Wednesday charged over corruption related to the multi-billion shilling Anglo Leasing scandal. Obure who was charged over crimes committed when he was a Minister of Finance in former President Daniel arap Moi’s government, was in the dock alongside former Transport and Communication Permanent Secretary Sammy Kyungu, former PS Ministry of Finance Joseph Magari and former PS for Internal Security and Provisional Administration Dave Mwangi. They have all denied abuse of office and conspiracy to commit economic crime charges, although Mwiraria and the Kamani’s who are represented by lawyer Ahmednassir Abdullahi were not in court/CFM NEWS Also charged alongside them were former Postmaster General Francis Chahonyo, former Finance Secretary Samuel Bundotich and David Onyonka who was in-charge of debt management in the Ministry of Finance at the time he is accused of committing economic crimes. David Mwiraria who...

MALLS ACROSS COUNTRY ON HIGH ALERT AFTER AL-QAEDA LINKED TERROR THREAT

A video purported to be by Somalia's al-Qaida-linked rebel group al-Shabab urged Muslims to attack shopping malls in the U.S., Canada, Britain and other Western countries. U.S. authorities said there was "no credible" evidence suggesting a U.S. mall attack was in the works. The threat by the al-Qaida affiliate came in the final minutes of a more than hourlong video released Saturday in which the extremists also warned Kenya of more attacks like the September 2013 assault on the Westgate Mall in Nairobi in which 67 people were killed. The masked narrator concluded by calling on Muslims to attack shopping malls, specifically naming the Mall of America in the Minneapolis suburb of Bloomington, as well as the West Edmonton Mall in Canada and the Westfield mall in Stratford, England. The authenticity of the video could not be immediately verified by The Associated Press. The FBI and Department of Homeland Security provided local law enforcement agencies and private sec...
kisii County News Thursday,June 18 2015 Father jailed for 30 years for killing son A signboard showing directions to Kisii law courts. A father was jailed for 30 years by the High Court in Kisii for killing his son. A man was jailed for 30 years by the High Court in Kisii after he was convicted of murdering his son. Kennedy Obara murdered his two and a half year old son, Hezbon Nyamongo by strangling him on April 11, 2013 at Nyaramba sub location in Gucha South, Kisii County. The court was told that Obara, who had a habit of beating his wife, had beaten her on the fateful night using a walking stick after which she fled to her parents at Suguta. She left behind her two sons who included the deceased and his seven-year-old brother. Kisii Resident Judge Ruth Sitati said that after carefully examining the evidence given by the prosecution and the cross examination, she concluded that it was Obara who killed the deceased. She said that in her considered view there was sufficient...